JINSI YA KU-DESIGN BLOG INAYOLIPA
----------------PART 2------------------
Tunaendelea na sehemu ya pili ya somo letu2. UNIQUENESS (UPEKEE)
Blog inayolipa lazima iwe ni ya kipekee (Unique). Hapa uwe makini kidogo maana hili ndilo lililo mhimu kuliko yote. Kama huwezi kumshawishi mtembeleaji mpya wa blog yako kuiona blog yako ni ya tofauti, nini kitamfanya aendelee kubaki hapo akisoma au arudi tena kesho kuona kama kuna jipya?
Njia pekee ya uhakika ya kuifanya blog yako ni tofauti na blog nyingine ni UPEKEE. Kama hakuna vitu vya kipekee kwenye blog yako usitegemee mtembeleaji wa kwanza au mpya wa blog yako kurudi tena au kuitafuta tena hiyo blog.
Ninaposema upekee kwenye blog naongelea vitu vikuu viwili ambavyo ni;
1. UNIQUE DESIGN/MUONEKANO WA KIPEKEE
Blog yako ili ilipe lazima iwe na muonekano wa kipekee. Muonekano wake kwa maana ya rangi, menu zake, namna inavyowasiliana na kujibizana na watembeleaji uwe ni wa kipekee na usiobadilika kila mara, mfano leo nimetembelea blog yako nakuta in background ya blue, kesho nakuta ina background nyekundu!, hapana, haiwi hivi. Unaweza kubadili muonekano wa blog yako baada ya miezi 6 au mwaka mmoja au miaka kadhaa, lakini siyo kila mara kwa sababu inaweza hata kuathiri kiasi cha uaminifu wa wasomaji wako kwako.
Hivyo unapofikiria kuanzisha blog yako fikiria pia juu ya kumpata mtengenezaji au designer wa blog atakayekutengenezea blog yenye muonekano wa pekee kwa maana kwamba blog yako haifanani fanani na blog nyingine kirahisi ili kukufanya wa tofauti.
2. UNIQUE CONTENT/MAKALA ZA KIPEKEE ORIJINO
Hapa ndiyo penye shida sana hasa kwa bloggers wengi wa Tanzania. Yaani Bloggers wengi wanachofanya ni kusubiri website ya gazeti fulani au blogger fulani aandike makala na wengine wote wana-copy na ku-paste kwenye blog zao kwa kichwa cha habari kile kile na maelezo yale yale!. Ni vigumu kuwa na blog inayolipa kwa staili hii.
Ili kuwa na Blog inayolipa, blogger unatakiwa ushiriki kwenye kutayarisha, kuandaa na kuandika makala za blog yako wewe mwenyewe. Sasa kuna sababu gani ya mimi kutembelea blog yako kama makala zako zote una-copy toka blog ya Shigongo?, ni heri nifunguwe kila siku blog ya Shigongo ambako nitapata orijino stori badala ya kuja kwako. Hii inaathari nyingi ikiwemo kukosa traffic kutoka search engines kama vile google.
Kuna vitu vingi sana unavyoweza kuviandika. Lakini wengi wanapenda kuandika tu juu ya mapenzi, michezo na siasa. Unaweza kuandika juu ya somo lolote iwe ni hesabu au biolojia, unaweza kuandika kuhusu kilimo, ufugaji, ujasiriamali, uchumi, afya, utalii, hoteli, shule, saikolojia, ushauri, malezi, na mengine mengi bila idadi na ukaeleimisha jamii inayokuzunguka.
Kwanini watu wanatembelea blog yako? Kwa sababu kuna jambo wanataka kusoma au kujifunza. Ukiwa blogger huna tofauti na mwalimu. Mwalimu au profesa wa chuo kikuu analipwa mshahara kwa sababu kuna kitu fulani anachofundisha.
Anzisha blog, chagua mada maalumu na udumu kwenye mada hiyo ukiifundisha kila mara kidogo kidogo. Andika habari au makala ambayo haifanani na wengine lakini yenye msaada kwa msomaji. Andika jambo likakamilika.
Kuna ushindani mkubwa na unaozidi kuongezeka siku hadi siku kwenye sekta hii ya uandishi. Andika kitu cha pekee (unique story) na mhimu kuliko yote, stori iwe ni yenye kumsaidia au kumuongezea thamani msomaji wako.
Kwa ufupi, sehemu hii ya pili inagusia kwenye jambo la UPEKEE, Upekee kwenye muonekano wa blog, kazi ambayo siyo yako wewe blogger bali ni kazi ya msanifu/designer wako na upekee kwenye
makala au stori zako, kazi ambayo ni yako moja kwa moja .
UVIVU ndilo neno pekee linaloweza kusomeka na likaleta maana ukianzia kulisoma upande wowote iwe ni kushoto au kulia.
sehemu ya 3
3. Self Hosted Blog
Ili blog au website ionekane hewani inahitaji vitu viwili
. Jina (Domain) <= tumeshajadili kuhusu domain hapo juu kwenye TLD
. stoo/hifadhi Host/Server (Host/Server)
Kama ilivyo kwa majina (domain), kuna majina ya bure na majina ya kulipia na tumeshajadili kwa kirefu hapo juu tofauti ya majina ya bure na majina ya kulipia na tukakubaliana kwamba ili uwe na blog inayolipa, unahitaji uwe na jina la kulipia na siyo la bure na sababu tumezieleza.
Hivyo hata stoo ya kuihifadhi hiyo blog ili ionekane hewani popote duniani zipo za aina mbili, za bure na za kulipia. Kwa kawaida kama ulifungulia blog yako kwenye google na ukabadili jina tu bila kubadili hifadhi (server/host) ya hiyo blog bado unahesabika unatumia stoo ya bure.
Kama ilivyo kwa bloggers wengi wanapoanza kuandika kwenye mtandao wengi huanza au hufikiri kutumia server za bure! Lakini ili upate mafanikio katika hiyo blog unalazimika kuwa na server ya kulipia.
Sehemu ya 3 ya vitu mhimu unavyohitaji ili kuwa na blog inayolipa inajikita kwenye Hosting/Server(Stoo).
Kwanini ulipie server?
Kwa sababu unapata uhuru zaidi na blog yako.
Kwa mfano ukiwa kwenye server za bure, mara nyingi
1. Utaambiwa idadi ya watu wanaoweza kutembelea hiyo blog yako kwa siku au kwa mwezi (bandwidth) ni wangapi. Usipolijuwa hili na ukafanya utundu wako siku 1 ukawapeleka watu 1000 au zaidi wakati umeambiwa kwenye hii server ya bure unaweza kuwa na wasomaji 200 tu kwa siku, lazima utaikuta blog yako ipo chini haionekani tena!.
Karibu sehemu ya Tatu na ya mwisho wa somo letu
NB: Kwa wewe unaehitaji kupata Blog inayolipa njoo 📩 0762647448-Sir Lemson au tia comment hapa 👇👇 ili tuende pamona...
Kikubwa umeelewa kunaza free domain na paid domain
Hvyo utachagua mwenyewe
Bei zangu ni sawa na bure tuu
KARIBU SANA
BY SIR LEMSON TECHNOLOGIES
Kikubwa umeelewa kunaza free domain na paid domain
Hvyo utachagua mwenyewe
Bei zangu ni sawa na bure tuu
KARIBU SANA
BY SIR LEMSON TECHNOLOGIES